Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Kamati ya katiba, sheria kujadili kesi 13 pamoja na ya mchezaji Hassan Kessy


Kamati ya Katiba, Sheria na Hadhi za wachezaji leo Jumamosi Septemba 24, 2016 itasikiliza mashauri 13.

Malalamiko hayo ni:

1.Mchezaji Ametre Richard ambaye atawasilisha mbele ya kamati makubaliano waliyokubaliana kukaa pamoja na kufikia mafaka.

2. Klabu ya Coastal Union dhidi ya Simba kuhusu madai ya fidia kwa wachezaji Hamad Juma na Abdi Banda.

3. Ally Rashid Ally dhidi ya Simba, malalamiko ya kunyimwa stahiki zake

4. Mchezaji Abdallah Juma dhidi ya Mbeya City, madai ya malimbikizo ya mshahara, fedha za usajili na gharama za matibabu.

5. Simba dhidi ya Young Africans, madai ni kuingia mkataba na mchezaji Hassan Kessy wakati ana mkataba na Klabu ya Simba

6. Kocha Abdul H. Banyai, kesi ni madai ya stahiki zake.

7. Coastal dhidi ya Young Africans, madai ya fidia ya matunzo ya mchezaji Juma Mahadhi

8. Saleh Malande dhidi ya Ndanda FC madai ya uvunjikaji wa mkataba

9. Coastal Union dhidi ya Mbeya City, madai ya fidia ya fidia kwa matunzo ya mchaji wao.

10. Sputanza FC dhidi ya Mbeya City, madai ya ada na usajili na mishahara

11. Kimondo FC dhidi ya Ruvu JKT, majibu ya kumalizana kati ya timu hizo mbili

12. Mathias Lule dhidi ya Stand United, taarifa ya kushindwa kufikia makubaliano ya kulipana.

13. Kimara United FC dhidi ya Kurugenzi FC, pingamizi la mchezaji Martine Sepeni kusajili timu ya Kurugenzi ya Iringa.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MUHIMBILI YAFANYA UPASUAJI KWA WATOTO WENYE TATIZO MFUMO WA HEWA NA NJIA YA MKOJO.

 Kutoka kulia ni Dk. Zaitun Bokhary  na Dk. Yona Ringo wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) wakimfanyia upasuaji mtoto mwenye tatizo kwenye mfumo wa hewa na chakula LEO kwa kushirikiana na  Profesa Saber  M. Waheeb (kushoto) na wenzake kutoka Misri.  Kutoka kulia ni Dk. Yona Ringo na  Dk. Zaitun Bokhary wa Muhimbili wakiendelea na upasuaji kwa kushirikiana na wataalamu kutoka Misri.  Profesa Saber  M. Waheeb (katikati) akijadiliana jambo na Dk. Zaitun Bokhary kabla ya kuanza kwa shughuli ya upasuaji kwa watoto wanane LEO. Kutoka kushoto ni Mwambata wa Jeshi la Wananchi Tanzania, Kanali Salum Haji Othman nchini Misri na nchi zote za Mashariki ya kati na Dk Yona Ringo wakifuatilia mazungumzo hayo leo.   Grace Joel akiwa na watoto wake pacha, Eliudi Joel  (katikati) na Elikana Joel wakisubiri kufanyiwa upasuaji wad njia ya mkono. Awali watoto hao kutoka Mbeya walizaliwa wakiwa wameungana na baadaye walifan...

SOMA BIBLIA TAKATIFU HAPA

                                                        BONYEZA HAPA KUSOMA BIBLIA       

AZAM ACADEMY MABINGWA MICHUANO YA AFRIKA MASHARIKI

TIMU ya vijana ya Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC ‘Azam FC Academy’, usiku wa leo imefanikiwa kuwa mabingwa wa michuano ya vijana ya Afrika Mashariki ‘Azam Youth Cup 2016’ baada ya kuichapa Ligi Ndogo Academy kutoka Kenya mabao 3-0, mchezo uliofanyika Uwanja wa Azam Complex. Azam Academy inatwaa ubingwa huo ikiwa imefikisha jumla ya pointi tisa baada ya kushinda mechi zote tatu ilizocheza nyingine zikiwa dhidi ya Future Stars Academy kutoka Arusha (4-1) na Football for Good Academy ya Uganda (5-1). Kikosi kizima cha Azam Academy na viongozi wao wakiwa na Kombe lao Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Saad Kawemba (kulia) akimkabidhi tuzo mchezaji Shaaban Iddi baada ya kuibuka mfungaji bora Shujaa wa mabingwa hao kwenye mchezo wa leo alikuwa ni mshambuliaji wake hatari Shaaban Idd aliyepachika wavuni mabao mawili kwa ustadi mkubwa dakika ya 15 na jingine 90, alilolifunga kwa staili ya ‘tik-tak’ huku bao jingine likifungwa na mshambuliaji mwingine hodari w...