Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Facebook yarejesha picha ya 'msichana wa Napalm'


Espen Egil Hansen ni mhariri wa gazeti la Aftenposten, Gazeti maarufu zaidi nchini NorwayAFTENPOSTEN/NICK UT 
Espen Egil Hansen ni mhariri wa gazeti la Aftenposten, Gazeti maarufu zaidi nchini Norway
Facebook imebatilisha uamuzi wake wa awali wa kufuta moja ya picha mashuhuri ya wakati wa vita vya Vietnam.
Picha hiyo inamuonyesha mtoto msichana aliyekuwa bila nguo akikimbia moto katika kijiji kimoja, katika shambulizi lililotekelezwa kwa kutumia kemikali ya napalm.
Facebook ilifuta picha hiyo kwa misingi kwamba ilikuwa ya uchi.
Facebook inasema imerejesha picha hiyo kutokana na umuhimu wake wa kihistoria.
Gazeti moja nchini Norway, Aftenposten, liliongoza shutuma dhidi ya Facebook, baada ya kampuni hiyo kufunga akaunti ya mmoja wa wanahabari wake, aliyetumia picha hiyo.
Mhariri wa gazeti la Afte-posten la Norway, amesema uamuzi wa Facebook kufuta picha hiyo inaonyesha wazi haiwezi kutofautisha kati ya picha za ponografia na zile zinazohusiana na historia ya matukio muhumu duniani.
Waziri mkuu wa Norway ambaye awali alichapisha picha hiyo kwenye akaunti yake kama ishara ya maandamano, amekaribisha uamuzi wa Facebook wa kurejesha picha hiyo.
Waziri mkuu wa Norway anasema uamuzi wa Facebook ulionyesha ushawishi mkubwa wa mitandao ya kijamii. Waziri mkuu wa Norway anasema uamuzi wa Facebook ulionyesha ushawishi mkubwa wa mitandao ya kijamii.
"wamefanya vizuri sana, mimi ni waziri mkuu aliye na furaha, inaonyesha kwamba matumizi ya mitandao ya kijamii yanaweza kuleta mabadiliko ya kisiasa, hata kwa mitandao ya kijamii yenyewe" Waziri mkuu Erna Solberg ameiambia BBC.

Msichana huyo ni nani?

Kim Phuc, alikuwa mwenye umri wa miaka 9 wakati picha hiyo ilipochukuliwa, akikimbia kuokoa maisha yake, baada ya shambulizi la Napalm, kaskazini mwa Saigon mwezi Juni 1972.
Alikumbwa na majeraha mabaya ya moto.
Mpiga picha Nick Ut na mwanahabari wa ITN Christopher Wain walimpeleka hospitalini.
Waliambiwa kwamba hakukuwa na matumaini kwamba msichana huyo angeendelea kuishi.
Facebook inasema imerejesha picha hii kutokana na umuhimu wake wa kihistoria.
Facebook inasema imerejesha picha hii kutokana na umuhimu wake wa kihistoria.
Baada ya kulazwa hospitalini kwa kipindi cha miezi 14, na kufanyiwa upasuaji mara 17 , aliruhusiwa kuenda nyumbani.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MUHIMBILI YAFANYA UPASUAJI KWA WATOTO WENYE TATIZO MFUMO WA HEWA NA NJIA YA MKOJO.

 Kutoka kulia ni Dk. Zaitun Bokhary  na Dk. Yona Ringo wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) wakimfanyia upasuaji mtoto mwenye tatizo kwenye mfumo wa hewa na chakula LEO kwa kushirikiana na  Profesa Saber  M. Waheeb (kushoto) na wenzake kutoka Misri.  Kutoka kulia ni Dk. Yona Ringo na  Dk. Zaitun Bokhary wa Muhimbili wakiendelea na upasuaji kwa kushirikiana na wataalamu kutoka Misri.  Profesa Saber  M. Waheeb (katikati) akijadiliana jambo na Dk. Zaitun Bokhary kabla ya kuanza kwa shughuli ya upasuaji kwa watoto wanane LEO. Kutoka kushoto ni Mwambata wa Jeshi la Wananchi Tanzania, Kanali Salum Haji Othman nchini Misri na nchi zote za Mashariki ya kati na Dk Yona Ringo wakifuatilia mazungumzo hayo leo.   Grace Joel akiwa na watoto wake pacha, Eliudi Joel  (katikati) na Elikana Joel wakisubiri kufanyiwa upasuaji wad njia ya mkono. Awali watoto hao kutoka Mbeya walizaliwa wakiwa wameungana na baadaye walifan...

SOMA BIBLIA TAKATIFU HAPA

                                                        BONYEZA HAPA KUSOMA BIBLIA       

AZAM ACADEMY MABINGWA MICHUANO YA AFRIKA MASHARIKI

TIMU ya vijana ya Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC ‘Azam FC Academy’, usiku wa leo imefanikiwa kuwa mabingwa wa michuano ya vijana ya Afrika Mashariki ‘Azam Youth Cup 2016’ baada ya kuichapa Ligi Ndogo Academy kutoka Kenya mabao 3-0, mchezo uliofanyika Uwanja wa Azam Complex. Azam Academy inatwaa ubingwa huo ikiwa imefikisha jumla ya pointi tisa baada ya kushinda mechi zote tatu ilizocheza nyingine zikiwa dhidi ya Future Stars Academy kutoka Arusha (4-1) na Football for Good Academy ya Uganda (5-1). Kikosi kizima cha Azam Academy na viongozi wao wakiwa na Kombe lao Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Saad Kawemba (kulia) akimkabidhi tuzo mchezaji Shaaban Iddi baada ya kuibuka mfungaji bora Shujaa wa mabingwa hao kwenye mchezo wa leo alikuwa ni mshambuliaji wake hatari Shaaban Idd aliyepachika wavuni mabao mawili kwa ustadi mkubwa dakika ya 15 na jingine 90, alilolifunga kwa staili ya ‘tik-tak’ huku bao jingine likifungwa na mshambuliaji mwingine hodari w...