Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Olimpiki Rio 2016: Matukio yaliyosisimua zaidi


Michezo ya Olimpiki Rio 2016 ilishuhudia matukio mengi ya kukumbukwa, baadhi mazuri na mengine mabaya. Haya hapa ni baadhi ya mambo yatakayokumbukwa sana.


Tonga
Mbeba bendera wa Tonga Pita Taufatofua alivutia wengi kwa mtindo wake wa mavazi sherehe ya ufunguzi.

Ragan Smith na Deandre Jordan
Picha moja iliyodhirisha tofauti katika kimo na unene ilikuwa hii ya mwanamichezo ya mazoezi ya viungo kutoka Marekani Ragan Smith na mchezaji mpira wa kikapu DeAndre Jordan.

Lee Goim na Hong Un Jong
Kulikuwa pia na kisa cha urafiki licha ya uadui wa mataifa. Lee Eun-ju wa Korea Kusini na Hong Un-jong wa Korea Kaskazini, wachezaji wawili wa mazoezi ya viungo ambao nchi zao ni mahasimu wakuu, walipiga picha pamoja.

Michael Phelps
Lakini hakukuwa na urafiki wakati wowote. Twitter 'iliwaka moto' baada ya bingwa wa uoegeleaji Michael Phelps kuonekana akimwangalia vibaya mpinzani wake Chad le Clos.

Rafaela Silva
Medali ya kwanza ya dhahau kwa wenyeji, iliyomwendea bingwa wa judo wa uzani wa kilo 57 Rafaela Silva, iliwapa kitulizo wakazi wa maeneo maskini Rio. Silva alizaliwa eneo maskini Rio na mwaka 2012 akatimuliwa mashindano London na kuelezwa kama "aibu kuu". Lakini mwaka huu ulikuwa wa fahari kwake.


Michael Phelpshelps, mwogeleaji aliyeshinda medali nyingi, hatimaye alitabasamu baada ya kumshinda Clos wa Afrika Kusini fainali za 200m butterfly wanaume. Baadhi walipendekeza Clos alifaa kuangazia kuogelea badala ya kumwangalia mpinzani wake.

Rami Anis

Kulikuwa na mengine mazuri kando na ushindi. Rami Anis, mwogeleaji wa timu ya wakimbizi aliyetoroka Syria 2015 kwa boti na kupitia bahari ya Mediterranean hadi Uturuki alisifiwa sana baada ya kuandikisha muda wake bora zaidi 100m freestyle upande wa wanaume.                                                                                picha zote kwa hisani ya bbc fwatialia zaidi kwenye bolg yako ya kijanja kwa taarifa mbalimbal  yoas.tz

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MUHIMBILI YAFANYA UPASUAJI KWA WATOTO WENYE TATIZO MFUMO WA HEWA NA NJIA YA MKOJO.

 Kutoka kulia ni Dk. Zaitun Bokhary  na Dk. Yona Ringo wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) wakimfanyia upasuaji mtoto mwenye tatizo kwenye mfumo wa hewa na chakula LEO kwa kushirikiana na  Profesa Saber  M. Waheeb (kushoto) na wenzake kutoka Misri.  Kutoka kulia ni Dk. Yona Ringo na  Dk. Zaitun Bokhary wa Muhimbili wakiendelea na upasuaji kwa kushirikiana na wataalamu kutoka Misri.  Profesa Saber  M. Waheeb (katikati) akijadiliana jambo na Dk. Zaitun Bokhary kabla ya kuanza kwa shughuli ya upasuaji kwa watoto wanane LEO. Kutoka kushoto ni Mwambata wa Jeshi la Wananchi Tanzania, Kanali Salum Haji Othman nchini Misri na nchi zote za Mashariki ya kati na Dk Yona Ringo wakifuatilia mazungumzo hayo leo.   Grace Joel akiwa na watoto wake pacha, Eliudi Joel  (katikati) na Elikana Joel wakisubiri kufanyiwa upasuaji wad njia ya mkono. Awali watoto hao kutoka Mbeya walizaliwa wakiwa wameungana na baadaye walifan...

SOMA BIBLIA TAKATIFU HAPA

                                                        BONYEZA HAPA KUSOMA BIBLIA       

AZAM ACADEMY MABINGWA MICHUANO YA AFRIKA MASHARIKI

TIMU ya vijana ya Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC ‘Azam FC Academy’, usiku wa leo imefanikiwa kuwa mabingwa wa michuano ya vijana ya Afrika Mashariki ‘Azam Youth Cup 2016’ baada ya kuichapa Ligi Ndogo Academy kutoka Kenya mabao 3-0, mchezo uliofanyika Uwanja wa Azam Complex. Azam Academy inatwaa ubingwa huo ikiwa imefikisha jumla ya pointi tisa baada ya kushinda mechi zote tatu ilizocheza nyingine zikiwa dhidi ya Future Stars Academy kutoka Arusha (4-1) na Football for Good Academy ya Uganda (5-1). Kikosi kizima cha Azam Academy na viongozi wao wakiwa na Kombe lao Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Saad Kawemba (kulia) akimkabidhi tuzo mchezaji Shaaban Iddi baada ya kuibuka mfungaji bora Shujaa wa mabingwa hao kwenye mchezo wa leo alikuwa ni mshambuliaji wake hatari Shaaban Idd aliyepachika wavuni mabao mawili kwa ustadi mkubwa dakika ya 15 na jingine 90, alilolifunga kwa staili ya ‘tik-tak’ huku bao jingine likifungwa na mshambuliaji mwingine hodari w...