Michezo ya Olimpiki Rio 2016
ilishuhudia matukio mengi ya kukumbukwa, baadhi mazuri na mengine
mabaya. Haya hapa ni baadhi ya mambo yatakayokumbukwa sana.
Mbeba bendera wa Tonga Pita Taufatofua alivutia wengi kwa mtindo wake wa mavazi sherehe ya ufunguzi.
Picha moja iliyodhirisha tofauti katika kimo na
unene ilikuwa hii ya mwanamichezo ya mazoezi ya viungo kutoka Marekani
Ragan Smith na mchezaji mpira wa kikapu DeAndre Jordan.
Kulikuwa pia na kisa cha urafiki licha ya uadui wa
mataifa. Lee Eun-ju wa Korea Kusini na Hong Un-jong wa Korea Kaskazini,
wachezaji wawili wa mazoezi ya viungo ambao nchi zao ni mahasimu wakuu,
walipiga picha pamoja.
Lakini hakukuwa na urafiki wakati wowote. Twitter
'iliwaka moto' baada ya bingwa wa uoegeleaji Michael Phelps kuonekana
akimwangalia vibaya mpinzani wake Chad le Clos.
Medali ya kwanza ya dhahau kwa wenyeji, iliyomwendea
bingwa wa judo wa uzani wa kilo 57 Rafaela Silva, iliwapa kitulizo
wakazi wa maeneo maskini Rio. Silva alizaliwa eneo maskini Rio na mwaka
2012 akatimuliwa mashindano London na kuelezwa kama "aibu kuu". Lakini
mwaka huu ulikuwa wa fahari kwake.
helps, mwogeleaji aliyeshinda medali
nyingi, hatimaye alitabasamu baada ya kumshinda Clos wa Afrika Kusini
fainali za 200m butterfly wanaume. Baadhi walipendekeza Clos alifaa
kuangazia kuogelea badala ya kumwangalia mpinzani wake.
Kulikuwa na mengine mazuri kando na ushindi. Rami
Anis, mwogeleaji wa timu ya wakimbizi aliyetoroka Syria 2015 kwa boti na
kupitia bahari ya Mediterranean hadi Uturuki alisifiwa sana baada ya
kuandikisha muda wake bora zaidi 100m freestyle upande wa wanaume. picha zote kwa hisani ya bbc fwatialia zaidi kwenye bolg yako ya kijanja kwa taarifa mbalimbal yoas.tz
Kutoka kulia ni Dk. Zaitun Bokhary na Dk. Yona Ringo wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) wakimfanyia upasuaji mtoto mwenye tatizo kwenye mfumo wa hewa na chakula LEO kwa kushirikiana na Profesa Saber M. Waheeb (kushoto) na wenzake kutoka Misri. Kutoka kulia ni Dk. Yona Ringo na Dk. Zaitun Bokhary wa Muhimbili wakiendelea na upasuaji kwa kushirikiana na wataalamu kutoka Misri. Profesa Saber M. Waheeb (katikati) akijadiliana jambo na Dk. Zaitun Bokhary kabla ya kuanza kwa shughuli ya upasuaji kwa watoto wanane LEO. Kutoka kushoto ni Mwambata wa Jeshi la Wananchi Tanzania, Kanali Salum Haji Othman nchini Misri na nchi zote za Mashariki ya kati na Dk Yona Ringo wakifuatilia mazungumzo hayo leo. Grace Joel akiwa na watoto wake pacha, Eliudi Joel (katikati) na Elikana Joel wakisubiri kufanyiwa upasuaji wad njia ya mkono. Awali watoto hao kutoka Mbeya walizaliwa wakiwa wameungana na baadaye walifan...
TIMU ya vijana ya Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC ‘Azam FC Academy’, usiku wa leo imefanikiwa kuwa mabingwa wa michuano ya vijana ya Afrika Mashariki ‘Azam Youth Cup 2016’ baada ya kuichapa Ligi Ndogo Academy kutoka Kenya mabao 3-0, mchezo uliofanyika Uwanja wa Azam Complex. Azam Academy inatwaa ubingwa huo ikiwa imefikisha jumla ya pointi tisa baada ya kushinda mechi zote tatu ilizocheza nyingine zikiwa dhidi ya Future Stars Academy kutoka Arusha (4-1) na Football for Good Academy ya Uganda (5-1). Kikosi kizima cha Azam Academy na viongozi wao wakiwa na Kombe lao Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Saad Kawemba (kulia) akimkabidhi tuzo mchezaji Shaaban Iddi baada ya kuibuka mfungaji bora Shujaa wa mabingwa hao kwenye mchezo wa leo alikuwa ni mshambuliaji wake hatari Shaaban Idd aliyepachika wavuni mabao mawili kwa ustadi mkubwa dakika ya 15 na jingine 90, alilolifunga kwa staili ya ‘tik-tak’ huku bao jingine likifungwa na mshambuliaji mwingine hodari w...
Maoni
Chapisha Maoni