Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mpiganaji wa Kiislamu Mali akiri makosa ICC

Mahdi akiwa mahakamani ICC
, 40, ni mshukiwa wa kwanza kukiri makosa ICC
Mpiganaji wa Kiislamu amekiri makosa ya kuharibu maeneo yenye umuhimu mkubwa kitamaduni katika mji wa Timbuktu, Mali baada ya kufikishwa katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita (ICC).
Ahmad al-Faqi al-Mahdi amesema anajutia vitendo vyake.
Ameshtakiwa kuongoza waasi ambao waliharibu turathi muhimu kihistoria mwaka 2012.
Hii ni mara ya kwanza kwa mpiganaji wa Kiislamu kufikishwa kortini katika ICC na pia mara ya kwanza kwa mshukiwa kukiri mashtaka.
Viongozi wa amshtaka wamesema Mahdi alikuwa mwanachama wa kundi la Kiislamu la Ansar Dine ambalo liliteka na kudhibiti mji wa Timbuktu kwa miezi kadha.
Waislamu huamini madhabahu pamoja na miswada ya kale ya mji huo ambayo huangazia mambo mengi yakiwemo historia na utaalamu wa nyota na sayari kuwa uabudu sanamu.
Nyaraka za mahakama zinamueleza Mahdi, 40, kama msomi wa kidini aliyewaongoza wapiganaji kutumia shoka na patasi kuharibu madhabahu hayo baada ya kushindwa kuwashawishi wakazi kuacha kuyatumia kama eneo la ibada.
Makaburi yakiharibiwa Timbuktu 
 Mahdi ameshtakiwa uharibifu uliotekelezwa katika makaburi tisa
Ameshtakiwa makosa ya uhalifu wa kivita kuhusiana na uharibifu uliotokea katika makarubi tisa na msikiti.
Mahdi ameambia ICC: "Ningependa kutoa ushauri wa Waislamu wote duniani, wasijihusishe na vitendo sawa na nilivyovifanya, kwa sababu havitakuwa na faida zozote kwa binadamu."
Baada yake kukiri makosa, huenda kesi yake ikamaliza kusikizwa kufikia mwisho wa wiki hii.
Anakabiliwa na adhabu ya kifungo cha hadi miaka 30 jela.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MUHIMBILI YAFANYA UPASUAJI KWA WATOTO WENYE TATIZO MFUMO WA HEWA NA NJIA YA MKOJO.

 Kutoka kulia ni Dk. Zaitun Bokhary  na Dk. Yona Ringo wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) wakimfanyia upasuaji mtoto mwenye tatizo kwenye mfumo wa hewa na chakula LEO kwa kushirikiana na  Profesa Saber  M. Waheeb (kushoto) na wenzake kutoka Misri.  Kutoka kulia ni Dk. Yona Ringo na  Dk. Zaitun Bokhary wa Muhimbili wakiendelea na upasuaji kwa kushirikiana na wataalamu kutoka Misri.  Profesa Saber  M. Waheeb (katikati) akijadiliana jambo na Dk. Zaitun Bokhary kabla ya kuanza kwa shughuli ya upasuaji kwa watoto wanane LEO. Kutoka kushoto ni Mwambata wa Jeshi la Wananchi Tanzania, Kanali Salum Haji Othman nchini Misri na nchi zote za Mashariki ya kati na Dk Yona Ringo wakifuatilia mazungumzo hayo leo.   Grace Joel akiwa na watoto wake pacha, Eliudi Joel  (katikati) na Elikana Joel wakisubiri kufanyiwa upasuaji wad njia ya mkono. Awali watoto hao kutoka Mbeya walizaliwa wakiwa wameungana na baadaye walifan...

SOMA BIBLIA TAKATIFU HAPA

                                                        BONYEZA HAPA KUSOMA BIBLIA       

AZAM ACADEMY MABINGWA MICHUANO YA AFRIKA MASHARIKI

TIMU ya vijana ya Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC ‘Azam FC Academy’, usiku wa leo imefanikiwa kuwa mabingwa wa michuano ya vijana ya Afrika Mashariki ‘Azam Youth Cup 2016’ baada ya kuichapa Ligi Ndogo Academy kutoka Kenya mabao 3-0, mchezo uliofanyika Uwanja wa Azam Complex. Azam Academy inatwaa ubingwa huo ikiwa imefikisha jumla ya pointi tisa baada ya kushinda mechi zote tatu ilizocheza nyingine zikiwa dhidi ya Future Stars Academy kutoka Arusha (4-1) na Football for Good Academy ya Uganda (5-1). Kikosi kizima cha Azam Academy na viongozi wao wakiwa na Kombe lao Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Saad Kawemba (kulia) akimkabidhi tuzo mchezaji Shaaban Iddi baada ya kuibuka mfungaji bora Shujaa wa mabingwa hao kwenye mchezo wa leo alikuwa ni mshambuliaji wake hatari Shaaban Idd aliyepachika wavuni mabao mawili kwa ustadi mkubwa dakika ya 15 na jingine 90, alilolifunga kwa staili ya ‘tik-tak’ huku bao jingine likifungwa na mshambuliaji mwingine hodari w...