Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMANNE 19.07.2016


Leicester City wanataka pauni milioni 45 kumuuza Riyad Mahrez, 25, lakini wana uhakika kuwa mchezaji huyo wa kimataifa wa Algeria atabakia King Power Stadium hasa baada ya kuondoka kwa N'Golo Kante kwenda Chelsea (Telegraph), Manchester United wamechelewesha kutangaza namba za jezi za wachezaji wake kwa msimu mpya mpaka watakapokamilisha usajili wa pauni milioni 105 wa kiungo wa Ufaransa na Juventus, Paul Pogba, 23 (Sun), mwenyekiti wa West Ham, David Sullivan, amesema mshambuliaji Diafra Sakho, 26, haondoki labda timu hiyo ipate mchezaji atakayeweza kuziba pengo lake (Mirror), Arsenal wanapanga kusajili wachezaji wawili kwenye safu ya ulinzi, wakimtaka Jason Denayer, 21 kutoka Manchester City na Matthias Ginter, 22 kutoka Borussia Dortmund (Sun), Bayern Munich na Real Madrid bado wanamfuatilia winga anayesakwa na Manchester City, Leroy Sane, 20, kwa mujibu wa baba wa mchezaji huyo kutoka Ujerumani (Manchester Evening News), dau la Arsenal la pauni milioni 2 limekubaliwa na Bolton la kumsajili beki Rob Holding, 20 (Daily Mail), meneja wa Hull City, Steve Bruce, amekuwa mtu wa pili kufanyiwa usaili wa kuwa meneja wa England, lakini anatarajiwa tu kupewa kazi hiyo iwapo Sam Allardyce hatokubaliana na maslahi yaliyopo (Daily Mail), Barcelona, Real Madrid, Manchester United na Chelsea zimepanda dau la kumtaka kiungo kutoka Ureno anayecheza Valencia, Andre Gomes, 22, anayedhaniwa kuwa na thamani ya pauni milioni 54 (Mundo Deportivo), Watford wanamfuatilia beki kutoka Ivory Coast Brice Dja Djedje, 25, kutoka Marseille (L'Equipe), Diego Costa, 27, hajaomba kuondoka Chelsea, na mshambuliaji huyo anatarajiwa kusalia Darajani msimu ujao (Evening Standard), meneja wa Chelsea Antonio Conte amekuwa na mawasiliano ya mara kwa mara na mshambuliaji wa Real Madrid, Alvaro Morata, 23, akimhakikishia nafasi yake iwapo ataamua kujiunga na Chelsea msimu ujao (Marca), meneja wa Everton Ronald Koeman, anamfuatilia kiungo wa Ureno na Sporting Lisbon William Carvalho, 24 (Mirror), Juventus wanakaribia kuwazidi kete AC Milan katika kumsajili winga kutoka Croatia, Marko Pjaka, 21, ambaye tayari ameaga wachezaji wenzake katika klabu ya Dinamo Zagreb (Gazzetta World), mshambuliaji wa zamani wa Manchester City Alvaro Negredo, 30, hatosafiri na timu yake ya Valencia kwenda Uholanzi, na badala yake atakwenda England kwa ajili ya vipimo vya afya kabla ya kujiunga na Middlesbrough (Gazzetta Live), Marseille wanafikiria kumchukua kwa mkopo mshambuliaji kutoka Cameroon, anayechezea Tottenham, Clinton N'Jie, 22, iwapo winga wao Georges-Kevin N'Koudou atakwenda White Hart Lane (Telegraph). Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MUHIMBILI YAFANYA UPASUAJI KWA WATOTO WENYE TATIZO MFUMO WA HEWA NA NJIA YA MKOJO.

 Kutoka kulia ni Dk. Zaitun Bokhary  na Dk. Yona Ringo wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) wakimfanyia upasuaji mtoto mwenye tatizo kwenye mfumo wa hewa na chakula LEO kwa kushirikiana na  Profesa Saber  M. Waheeb (kushoto) na wenzake kutoka Misri.  Kutoka kulia ni Dk. Yona Ringo na  Dk. Zaitun Bokhary wa Muhimbili wakiendelea na upasuaji kwa kushirikiana na wataalamu kutoka Misri.  Profesa Saber  M. Waheeb (katikati) akijadiliana jambo na Dk. Zaitun Bokhary kabla ya kuanza kwa shughuli ya upasuaji kwa watoto wanane LEO. Kutoka kushoto ni Mwambata wa Jeshi la Wananchi Tanzania, Kanali Salum Haji Othman nchini Misri na nchi zote za Mashariki ya kati na Dk Yona Ringo wakifuatilia mazungumzo hayo leo.   Grace Joel akiwa na watoto wake pacha, Eliudi Joel  (katikati) na Elikana Joel wakisubiri kufanyiwa upasuaji wad njia ya mkono. Awali watoto hao kutoka Mbeya walizaliwa wakiwa wameungana na baadaye walifan...

SOMA BIBLIA TAKATIFU HAPA

                                                        BONYEZA HAPA KUSOMA BIBLIA       

AZAM ACADEMY MABINGWA MICHUANO YA AFRIKA MASHARIKI

TIMU ya vijana ya Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC ‘Azam FC Academy’, usiku wa leo imefanikiwa kuwa mabingwa wa michuano ya vijana ya Afrika Mashariki ‘Azam Youth Cup 2016’ baada ya kuichapa Ligi Ndogo Academy kutoka Kenya mabao 3-0, mchezo uliofanyika Uwanja wa Azam Complex. Azam Academy inatwaa ubingwa huo ikiwa imefikisha jumla ya pointi tisa baada ya kushinda mechi zote tatu ilizocheza nyingine zikiwa dhidi ya Future Stars Academy kutoka Arusha (4-1) na Football for Good Academy ya Uganda (5-1). Kikosi kizima cha Azam Academy na viongozi wao wakiwa na Kombe lao Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Saad Kawemba (kulia) akimkabidhi tuzo mchezaji Shaaban Iddi baada ya kuibuka mfungaji bora Shujaa wa mabingwa hao kwenye mchezo wa leo alikuwa ni mshambuliaji wake hatari Shaaban Idd aliyepachika wavuni mabao mawili kwa ustadi mkubwa dakika ya 15 na jingine 90, alilolifunga kwa staili ya ‘tik-tak’ huku bao jingine likifungwa na mshambuliaji mwingine hodari w...