Ruka hadi kwenye maudhui makuu

RENATO SANCHES ASHINDA TUZO YA MCHEZAJI CHIPUKIZI EURO 2016


Mchezaji kinda Renato Sanches ametajwa kuwa mchezaji bora kijana wa fainali za Ulaya (Euro 2016) ambazo zilifikia tamati usiku wa kuamkia hii leo jijini Paris nchini Ufaransa.
Kiungo huyo ambaye ni kinda akatika michuano hiyo ya (Euro 2016) ameshinda tuzo hiyo na kuwashinda wenzake Kingsley Coman wa Ufaransa na Mreno mwenzie Raphael Guerreiro.
Zawadi hizo ambazo zilikuwa maalum kwa wale wote waliozaliwa baada ya January 1 1994, zilitolewa na jopo la Wataalamu wa masuala ya Kiufundi wa UEFA lililokuwa likiongozwa na Lupescu. Wengine waliokuwa kwenye jopo hilo ni Sir Alex Ferguson na Alain Giresse.
Sanches alianza kuonesha uwezo wake pale tu alipopewa nafasi kwenye mchezo dhidi ya Poland na kuonesha kiwango bora kabisa kilichomshawishi kocha wake kumuanzisha kwenye mechi zilizofuata.
Sanches alifunga goli lake la kwanza kwa timu yake katika mchezo dhidi ya Poland na kumfanya kuwa mchezaji wa tatu kijana kucheza mchezo wa fainali ya Euro mwaka huu.
Alikuwepo kwenye michezo yote muhimu ambayo Ureno walipata ushindi, ambayo ni dhidi ya Wales ambapo walishinda 2-0 na jana dhidi ya Ufaransa na kumfanya kushinda tuzo hiyo katika umri mdogo zaidi wa miaka 18 na siku 328.
Kinda huyo mzaliwa wa Lisbon, ambaye kwenye dirisha hili la usajili amejiunga na FC Bayern München akitokea Benfica kwa ada ya awali ya uero milioni 35, alianza msimu wa 2015/16 akiwa na timu B ya Benfica na kushiriki katika Michuano ya Ligi ya Vijana ya UEFA, Michezo ya kufuzu Michuano ya Ulaya kwa vijana chini ya miaka 19 na vile vile Ligi ya Mabingwa Ulaya kabla ya kupata nafasi ya kucheza timu ya taifa ya Ureno kwa mara ya kwanza Machi 25 mwaka huu.
Renato Sanches na Kingsley Coman msimu ujao watakuwa wote kwenye klabu ya Bayern huku Raphael Guerreiro naye atakuwa katika klabu ya Borussia Dortmund ya Ujerumani.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MUHIMBILI YAFANYA UPASUAJI KWA WATOTO WENYE TATIZO MFUMO WA HEWA NA NJIA YA MKOJO.

 Kutoka kulia ni Dk. Zaitun Bokhary  na Dk. Yona Ringo wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) wakimfanyia upasuaji mtoto mwenye tatizo kwenye mfumo wa hewa na chakula LEO kwa kushirikiana na  Profesa Saber  M. Waheeb (kushoto) na wenzake kutoka Misri.  Kutoka kulia ni Dk. Yona Ringo na  Dk. Zaitun Bokhary wa Muhimbili wakiendelea na upasuaji kwa kushirikiana na wataalamu kutoka Misri.  Profesa Saber  M. Waheeb (katikati) akijadiliana jambo na Dk. Zaitun Bokhary kabla ya kuanza kwa shughuli ya upasuaji kwa watoto wanane LEO. Kutoka kushoto ni Mwambata wa Jeshi la Wananchi Tanzania, Kanali Salum Haji Othman nchini Misri na nchi zote za Mashariki ya kati na Dk Yona Ringo wakifuatilia mazungumzo hayo leo.   Grace Joel akiwa na watoto wake pacha, Eliudi Joel  (katikati) na Elikana Joel wakisubiri kufanyiwa upasuaji wad njia ya mkono. Awali watoto hao kutoka Mbeya walizaliwa wakiwa wameungana na baadaye walifan...

SOMA BIBLIA TAKATIFU HAPA

                                                        BONYEZA HAPA KUSOMA BIBLIA       

AZAM ACADEMY MABINGWA MICHUANO YA AFRIKA MASHARIKI

TIMU ya vijana ya Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC ‘Azam FC Academy’, usiku wa leo imefanikiwa kuwa mabingwa wa michuano ya vijana ya Afrika Mashariki ‘Azam Youth Cup 2016’ baada ya kuichapa Ligi Ndogo Academy kutoka Kenya mabao 3-0, mchezo uliofanyika Uwanja wa Azam Complex. Azam Academy inatwaa ubingwa huo ikiwa imefikisha jumla ya pointi tisa baada ya kushinda mechi zote tatu ilizocheza nyingine zikiwa dhidi ya Future Stars Academy kutoka Arusha (4-1) na Football for Good Academy ya Uganda (5-1). Kikosi kizima cha Azam Academy na viongozi wao wakiwa na Kombe lao Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Saad Kawemba (kulia) akimkabidhi tuzo mchezaji Shaaban Iddi baada ya kuibuka mfungaji bora Shujaa wa mabingwa hao kwenye mchezo wa leo alikuwa ni mshambuliaji wake hatari Shaaban Idd aliyepachika wavuni mabao mawili kwa ustadi mkubwa dakika ya 15 na jingine 90, alilolifunga kwa staili ya ‘tik-tak’ huku bao jingine likifungwa na mshambuliaji mwingine hodari w...