Vikosi vya usalama
nchini Uturuki vinasema kuwa zaidi ya maafisa 8,000 wa polisi
wamefutwa kazi, kufuatia jaribio la mapinduzi lililozimwa wiki
iliyopita.
Runinga rasmi ya serikali nchini Uturuki- Anadolu,
inasema kuwa maafisa wengine waliokamatwa ni pamoja na majenerali wakuu
wa kijeshi.
Takriban wanajeshi elfu 6,000 na wahudumu wa mahakama nao pia wamekamatwa.
Fethullah Gulen amekanusha madai ya kuchochea mapinduzi
Vyombo vya habari vinasema kuwa maafisa hao
wanalaumiwa kwa kuwa na uhusiano na mapinduzi hayo ambayo serikali
inadai kuwa yalipangwa na kiongozi wa dini aliyeko uhamishoni nchini
Marekani- Fethullah Gulen.
Msako dhidi ya maafisa wa usalama waliohusika na mipango ya kuipindua serikali juma lililopita nchini Uturuki, unaendelea.
Kituo cha mafunzo ya wanajeshi wa angani mjini cha Istanbul, kilivamiwa na maafisa kukamatwa.
Usiku wa kuamkia leo na mapema Jumatatu alfajiri,
zaidi ya maafisa elfu nane 8,000 wa polisi walikamatwa kushauriwa
kuwasilisha bunduki zao na kusimamishwa kazi.
Kituo cha mafunzo ya wanajeshi wa angani mjini cha Istanbul, kilivamiwa na maafisa hao kukamatwa.
Waendesha
mashtaka wameanza kuwahoji kinara mkuu wa jaribio hilo la mapinduzi
ambaye alikuwa kamanda mkuu wa jeshi la angani Akin Ozturk, ambaye ni
miongoni mwa makamanda wakuu 100 waliokamatwa.
Takriban wanajeshi elfu 6,000 na wahudumu wa mahakama nao pia wamekamatwa.
Maafisa wanane wa kijeshi walioingia nchini Ugiriki
kwa kutumia Helikopta, wamefikishwa mahakamani katika mji ulioko mpakani
wa Alexandrou-poli, ili kushtakiwa kwa kuingia nchini humo bila idhini.
Uturuki imeomba Ugiriki kuwarejesha nyumbani ili kushtakiwa, lakini mawakili wao wameomba idhini ya uhamiaji.
Kutoka kulia ni Dk. Zaitun Bokhary na Dk. Yona Ringo wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) wakimfanyia upasuaji mtoto mwenye tatizo kwenye mfumo wa hewa na chakula LEO kwa kushirikiana na Profesa Saber M. Waheeb (kushoto) na wenzake kutoka Misri. Kutoka kulia ni Dk. Yona Ringo na Dk. Zaitun Bokhary wa Muhimbili wakiendelea na upasuaji kwa kushirikiana na wataalamu kutoka Misri. Profesa Saber M. Waheeb (katikati) akijadiliana jambo na Dk. Zaitun Bokhary kabla ya kuanza kwa shughuli ya upasuaji kwa watoto wanane LEO. Kutoka kushoto ni Mwambata wa Jeshi la Wananchi Tanzania, Kanali Salum Haji Othman nchini Misri na nchi zote za Mashariki ya kati na Dk Yona Ringo wakifuatilia mazungumzo hayo leo. Grace Joel akiwa na watoto wake pacha, Eliudi Joel (katikati) na Elikana Joel wakisubiri kufanyiwa upasuaji wad njia ya mkono. Awali watoto hao kutoka Mbeya walizaliwa wakiwa wameungana na baadaye walifan...
TIMU ya vijana ya Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC ‘Azam FC Academy’, usiku wa leo imefanikiwa kuwa mabingwa wa michuano ya vijana ya Afrika Mashariki ‘Azam Youth Cup 2016’ baada ya kuichapa Ligi Ndogo Academy kutoka Kenya mabao 3-0, mchezo uliofanyika Uwanja wa Azam Complex. Azam Academy inatwaa ubingwa huo ikiwa imefikisha jumla ya pointi tisa baada ya kushinda mechi zote tatu ilizocheza nyingine zikiwa dhidi ya Future Stars Academy kutoka Arusha (4-1) na Football for Good Academy ya Uganda (5-1). Kikosi kizima cha Azam Academy na viongozi wao wakiwa na Kombe lao Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Saad Kawemba (kulia) akimkabidhi tuzo mchezaji Shaaban Iddi baada ya kuibuka mfungaji bora Shujaa wa mabingwa hao kwenye mchezo wa leo alikuwa ni mshambuliaji wake hatari Shaaban Idd aliyepachika wavuni mabao mawili kwa ustadi mkubwa dakika ya 15 na jingine 90, alilolifunga kwa staili ya ‘tik-tak’ huku bao jingine likifungwa na mshambuliaji mwingine hodari w...
Maoni
Chapisha Maoni