Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TFDA YAKAMATA ZAIDI YA TANI SITA ZA TENDE ZILIZO HIFADHIWA KWENYE MADEBE


Mamlaka ya chakula na dawa nchini tawi la Horohoro mpakani mwa Kenya na Tanzania imekamata shehena ya bidhaa aina ya tende zaidi ya tani sita zilizokuwa zikitokea uarabuni kupitia nchi jirani ya Kenya kufuatia bidhaa hizo zilizokuwa zikiletwa nchini kwa ajili ya matumizi ya mwezi Mtukufu wa Ramadhani kuhifadhiwa katika madebe yanayodaiwa kuwa yanaweza kuleta madhara kwa mtumiaji.

Akizungumza na ITV katika eneo la Horohoro mpakani mwa  Kenya na Tanzania mkaguzi wa mamlaka hiyo katika mpaka huo Thomas Nkondola amesema zipo baadhi ya tende ambazo zinaingizwa kutoka uarabuni kupitia nchi jirani ya Kenya zinakuwa na nembo ya ubora na kufungashwa katika vifungashio ambavyo havina madhara na wanaziruhusu tofauti na hizo zilizokamatwa.

Baadhi ya watumiaji wa bidhaa hiyo ya tende waliokutwa katika mpaka huo wamesema baadhi yao walitumia tende zilizofungashwa katika madebe waliathirika afya zao kwa kushikwa na homa za matumbo hatua ambayo wameshauriwa na daktari kuwa bidhaa hiyo isitumike kwa matumizi ya binadamu.

Kufuatia hatua hiyo mkaguzi mkuu wa (TFDA) tawi la Horohoro Bwana Nkondola amewashauri watumiaji kuwa makini na bidhaa aina ya tende ambazo zimeingizwa katika njia zisizo rasmi huku mamlaka hiyo ikiendelea kuzuia zile ambazo zimehifadhiwa katika madebe ambayo yanahifadhi kutu ambayo ni hatari kwa afya ya mtumiaji.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MUHIMBILI YAFANYA UPASUAJI KWA WATOTO WENYE TATIZO MFUMO WA HEWA NA NJIA YA MKOJO.

 Kutoka kulia ni Dk. Zaitun Bokhary  na Dk. Yona Ringo wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) wakimfanyia upasuaji mtoto mwenye tatizo kwenye mfumo wa hewa na chakula LEO kwa kushirikiana na  Profesa Saber  M. Waheeb (kushoto) na wenzake kutoka Misri.  Kutoka kulia ni Dk. Yona Ringo na  Dk. Zaitun Bokhary wa Muhimbili wakiendelea na upasuaji kwa kushirikiana na wataalamu kutoka Misri.  Profesa Saber  M. Waheeb (katikati) akijadiliana jambo na Dk. Zaitun Bokhary kabla ya kuanza kwa shughuli ya upasuaji kwa watoto wanane LEO. Kutoka kushoto ni Mwambata wa Jeshi la Wananchi Tanzania, Kanali Salum Haji Othman nchini Misri na nchi zote za Mashariki ya kati na Dk Yona Ringo wakifuatilia mazungumzo hayo leo.   Grace Joel akiwa na watoto wake pacha, Eliudi Joel  (katikati) na Elikana Joel wakisubiri kufanyiwa upasuaji wad njia ya mkono. Awali watoto hao kutoka Mbeya walizaliwa wakiwa wameungana na baadaye walifan...

SOMA BIBLIA TAKATIFU HAPA

                                                        BONYEZA HAPA KUSOMA BIBLIA       

AZAM ACADEMY MABINGWA MICHUANO YA AFRIKA MASHARIKI

TIMU ya vijana ya Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC ‘Azam FC Academy’, usiku wa leo imefanikiwa kuwa mabingwa wa michuano ya vijana ya Afrika Mashariki ‘Azam Youth Cup 2016’ baada ya kuichapa Ligi Ndogo Academy kutoka Kenya mabao 3-0, mchezo uliofanyika Uwanja wa Azam Complex. Azam Academy inatwaa ubingwa huo ikiwa imefikisha jumla ya pointi tisa baada ya kushinda mechi zote tatu ilizocheza nyingine zikiwa dhidi ya Future Stars Academy kutoka Arusha (4-1) na Football for Good Academy ya Uganda (5-1). Kikosi kizima cha Azam Academy na viongozi wao wakiwa na Kombe lao Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Saad Kawemba (kulia) akimkabidhi tuzo mchezaji Shaaban Iddi baada ya kuibuka mfungaji bora Shujaa wa mabingwa hao kwenye mchezo wa leo alikuwa ni mshambuliaji wake hatari Shaaban Idd aliyepachika wavuni mabao mawili kwa ustadi mkubwa dakika ya 15 na jingine 90, alilolifunga kwa staili ya ‘tik-tak’ huku bao jingine likifungwa na mshambuliaji mwingine hodari w...